Friday, September 30, 2011

SIKIA MPINI WA 'NGWIJI' DIBLO DIBALA, MPIGA GITAA LA 'SOLO' NAMBA MOJA BARANI AFRICA...

HII NI RIPOTI MAALUM YA UKWELI NA TUNAOMBA HAYA MAMBO YASHUGHULIKIWE NA WAHUSIKA JAMANI...



WIKI iliyopita mfungwa aliyemaliza kifungo chake alieleza kwa kina jinsi alivyoingiza simu na bangi gerezani na kuzitumia kama mradi wake wa kujipatia pesa. Pia watu wengine wawili waliowahi kufungwa katika magereza ya Segerea, Mwanga na Karanga mkoani Kilimanjaro nao wameeleza jinsi walivyokuwa wakitoa pesa kupewa chakula kizuri gerezani.

Biashara ya chakula
Mmoja wa watu hao alisema: “Ukitaka kupata chakula kizuri katika Gereza la Segerea ilikuwa lazima ununue kutoka kwa wapishi.

“Unachoweza kukifanya ni kuzungumza nao halafu unawalipa kwa wiki. Chakula ambacho unaweza kukipata ukiingia mkataba huo ni mboga iliyoungwa kwa mafuta na ugali”.

Anasema kama huna cha kuwapa kwa wiki hiyo unaweza kuwasiliana na ndugu yako akampa fedha mmoja wa askari magereza wanaopeleka mahabusu mahakamani akaziingiza magereza.

Mtu mwingine ambaye ameonja kifungo katika gereza la Karanga na Mwanga mkoani Kilimanjaro alisema; “Rushwa ndani ya magereza ni kubwa kiasi kwamba, ukiwa huna pesa ya kuhonga askari, mnyapara au daktari wa magereza, utakiona kifungo kibaya mno”.

Akisimulia jinsi alivyoingiza simu magereza, Mfungwa huyo ambaye alitumikia kifungo cha miaka minne katika magereza mkoani Kilimanjaro, alisema aliingiza simu gerezani baada ya kushuhudia askari mmoja wa magereza akimpiga mfungwa ambaye baadaye alifariki dunia.

Kutokana na tukio hilo, askari huyo baada ya kuambiwa na baadhi ya wafungwa kuwa aliyeshuhudia tukio hilo ana uwezo wa kuvujisha taarifa hiyo kwa watu wengine nje ya gereza aliamua kujenga naye urafiki.

Anasema askari hiyo alimwahidi kuwa atamsaidia kuingiza simu gerezani ambayo aliitumia muda wote kuwasiliana na mke wake na marafiki zake.

Alisema, "Simu hiyo ilinisaidia kupata habari za kila siku za familia yangu na pia niliwapigia watu mbalimbali bila matatizo,"

Mfungwa huyo, anasema uhalifu unaofanywa na askari magereza ndio unaosababisha kutoa mwanya kwa wafungwa wa kiume kujiingiza katika vitendo vya kuvunja sheria, ikiwamo kuingiza bangi, simu na kufanya mapenzi na wanawake wa nje ya gereza.

Anasema wakati mwingine askari magereza wanashirikiana na wafungwa kuiba mali za gereza, ikiwamo mahindi na mbolea na kuuza uraiani.

Anatoa mfano kuwa, kuna siku alishirikishwa na askari mmoja katika Gereza la Karanga kuiba magunia saba ya mahindi.Alifahamisha kuwa waliyapakia katika lori kwenda kupanda shamba la gereza, lakini badala yake waliyauza kwa watu waliokubaliana na askari huyo.

Alidai kuwa baada ya kuuza alipata mgawo wake pamoja na wafungwa wenzake wanne waliokuwamo ndani ya gari hilo.

Mbali ya kushirikishwa katika wizi huo wa mahindi ya magereza, pia alidai kuwa wahi kutumiwa na askari huyo kuiba mbolea ya ruzuku ambazo zinatolewa na serikali kwa gereza hilo.

Vilevile, kwa kushirikiana na baadhi ya askari magereza alisema aliwahi kuingiza vitu mbalimbali gerezani ikiwamo pesa na bangi kwa ajili ya kuiuza.


Kuhusu kufanya mapenzi na wanawake nje ya magereza, alisema hilo ni jambo linalowezekana kabisa. Anasema wafungwa wengi wenye uwezo huwapa pesa askari wasiokuwa na maadili hivyo kupangiwa kufanya kazi nje ya gereza.

Alisema: "Unachotakiwa kufanya ni kupanga na askari magereza ambaye anampa taarifa mke wako kuwa mtakuwa wapi."

Mfungwa huyo anasema: Akifika mke wako, askari magereza anakuruhusu kwenda sehemu yoyote ya kificho karibu na eneo hilo.Alifahamisha njia nyingine ambayo inaweza kukufanya ukutane na mke wako ni kwenda kulazwa hospitalini.

“Asilimia kubwa ya wafungwa wanaolazwa hospitali huwa sio wagonjwa, bali hupata kibali cha kwenda kutibiwa baada ya kutoa chochote kwa daktari wa gereza,” alifahamisha na kuongeza."Usione ndugu yangu wafungwa wengi wamelazwa hospitalini, wengine wanakuwa sio wagonjwa, wapo huko kupumzika na kupata nafasi ya kuonana na ndugu zao kirahisi,"

Alieleza kuwa: “Ukipata kibali cha kwenda kutibiwa hospitali, unaweza kumpa chochote askari anayekulinda akakuruhusu kukutana na mkeo usiku.

Vilevile, sehemu nyingine ambayo mfungwa anaweza kuitumia kukutana na mke wake ni pale anapopangiwa kufanya kazi kwenye mashamba ya maafisa wa magereza ambako hupata uhuru zaidi.

"Mfungwa kufanya kazi kwenye mashamba ya maafisa wa magereza ni kosa ndiyo maana wanapokuchukua huwa wanatoa uhuru kiasi, hasa kwa wafungwa wanaokaribia kumaliza vifungo, au wenye tabia njema," alifahamisha.

Hata hivyo alisema, ingawa kuna wafungwa ambao wapo hospitali kwa ajili ya kuishi vyema, wapo wafungwa ambao wanaumwa ambao wanahitaji kupatiwa matibabu, lakini hawapelekwi hospitalini.

Alidai kuwa kuna usanii mwingi katika magereza, kwani hata Tume ya Haki za Binadamu wanapopita kuangalia hali za wafungwa baadhi ya viongozi wa magereza hutandika mashuka mapya katika magodoro ya wafungwa, lakini wakiondoka tu huyaondoa haraka.

Ripoti ya Tume
Ripoti ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ya mwaka 2009/2010 imeonyesha kuwa chakula kikuu katika magereza nchini ni ugali na maharage. Mboga za majani, nyama, wali na matunda huliwa baadhi ya siku katika wiki.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, ilibainika kuwa asimilia 59.2 ya wafungwa waliohojiwa walikiri kuwa chakula kinatosha kama kitasimamiwa na kuboreshwa huku asilimia 40 walikiri kuwa chakula hakitoshi.

Tume inapendekeza kuondolewa kwa matumizi ya mitondoo magerezani kwani hali hii imejitokeza zaidi katika mabweni ya wafungwa wa kunyongwa mfano gereza la Isanga, Ukonga, Uyui na Gereza la Mahabusu la Morogoro.

Tume inashauri upekuzi wa wafungwa kwa kuwavua nguo hadharani utafutiwe njia mbadala kwa vile utaratibu wa sasa unavunja haki ya faragha na staha ya mtu.

Aidha, kuna fursa ya kutembelewa na ndugu zao na kuonana nao ana kwa ana. Magereza yote yametayarisha sehemu maalumu na taratibu za kufuatwa wakati wafungwa na mahabusu wanapowasiliana na jamaa zao.

Msemaji Magereza
Hata hivyo, wiki iliyopita Msemaji wa Jeshi la Magereza, Mtiga Omari alisema kuwa jeshi lake limekuwa likipambana na vitendo hivyo viovu na kwamba wapo watu wengi wakiwamo raia na wafungwa ambao wamefunguliwa kesi za kuwasaidia wafungwa kumiliki simu gerezani.

Mtiga alisema jeshi hilo lina mambo mengi ambayo wananchi wanapaswa kuyajua, lakini atayazungumzia kwa ruksa ya Kamishina wa Magereza, Augustine Nanyaro.


MJUE VAN VICKER, MWIGIZAJI ANAYEPIGWA VITA NCHINI NIGERIA HIVISASA...


Huyu jamaa anaitwa JOSEPH VAN VICKER! Ni mwigizaji maarufu wa Movie za Kinigeria anayejulikana sana Barani Africa! Baba yake ni Mholanzi na mama yake ni Mghana. Baba yake alifariki Dunia wakati Van Vicker akiwa na umri wa miaka 6 na kuanzia hapo alilelewa na mama yake mpaka alipokuwa na uwezo wa Kujitegemea! Jamaa ameshanyakuwa Tuzo kibao za Filamu na pia inasemekana baada ya yeye kutoka kwao Ghana na kuhamishia kazi zake za Filamu nchini Nigeria na kukumbana na Ubaguzi mkali kwa wadau wa Filamu na hasa waigizaji wa Nollywood waliodhani aatawafunika na kweli 'AKAWAFUNIKA' kweli na hata waigiza maarufu wa kimume nchini humo kama vile RAMSEY NOAH, JIMMY IYKE na wengineo jasho linawatoka sasa...

Hobbies za huyu jamaa ni kucheza Football, Table tennis na kuogelea...

MCHEC VAN VICKER KWENYE KIPANDE HIKI SASA...

Thursday, September 29, 2011


Mwigizaji huyu anayependwa sana na wakina Dada ameshaoa jamani na amejaaliwa kupata watoto 3! Kwaiyo kama kuna siku ulikuwa na ndoto 'MBAYA' na yeye basi imekula kwako...

JAMAA PIA NI LULU KWENYE MATANGAZO YA BIASHARA, MCHEC HAPA...

KWA YALIYOTOKEA ZAMBIA JUZI NI MFANO WA KUINGWA NA VIONGOZI WOTE WA AFRICA...


Huyu ndie Rais mpya wa Zambia Mh. MICHAEL SATA, na hapa ni wakati anaapishwa juzi kushika Madaraka mapya ya kuiongoza nchi hiyo...

Na huyu ndie Rais aliyemaliza muda wake Mh. RUPIA BANDA.
RAIS mpya wa Zambia, Michael Sata aapishwa na kuahidi kupambana na ufisadi na umasikini nchini humo.
Akihutubia baada ya hafla ya kuapishwa, Sata ambaye ni kiongozi wa chama cha cha Patriotic Front (PF) ambaye pia anajulikana kwa umaarufu kwa jina la ‘King Cobra’ ameahidi kupambana na umasikini na ufisadi aliouita kuwa ni maradhi ambayo yanapaswa kupatiwa tiba.

‘King Cobra’, ameapishwa rasmi mjini Lusaka kuwa rais mpya wa nchi hiyo baada ya kushinda katika uchaguzi dhidi ya rais anayeondoka Rupiah Banda.Banda ambaye alikuwa aamini machoni mwake kwa kilichotokea, alitoa hotuba yakukubali matokeo hayo huku akiwa anabubujikwa na machozi mbele ya waandishi wa habari.

“Watu wa Zambia wamezungumza na lazima sote tusikilize," Banda alisema maneno hayo kwa hudhuni huku akiwa anafuta machozi baada ya kumaliza kutoa hotuba yake.Banda aliongeza kuwa, "Nikizungumza kwa nafsi yangu na chama changu, tunakubali matokeo. Sisi ni chama cha kidemokrasia na hakuna namna nyingine yeyote ile."

Habari zinasema kuwa, chama cha Movement for Multiparty Democracy (MMD) kilichokuwa kinaongozwa na Banda kimekuwepo madarakani nchini Zambia kwa miaka 20.

Sata ambaye anajulikana kwa umaarufu ‘King Cobra’, ni kiongozi wa chama cha Patriotic Front (PF) ambaye ana umri wa miaka 74, baada ya kuapishwa alisema kuwa, wawekezaji wa kigeni wanakaribishwa katika taifa hilo la Afrika lililo na utajiri wa madini ya shaba, ili mradi tu watii sheria za ajira nchini humo.

Sata ana ungwaji mkono mkubwa katika eneo hilo la uchimbaji madini ambapo amewalaumu wakurugenzi wa China kuwatumia vibaya, kuwanyanyasa na kuwapa malipo kidogo wafanyakazi nchini humo.

Zaidi ya asilimia 60 ya wananchi wa Zambia wanaishi chini ya kipato cha dola mbili kwa siku.Siku ya Alhamisi, kulikuwa na ghasia eneo la Kaskazini lenye migodi zilizofanywa na wanaounga mkono upinzani wakiwa hawana subra na matokeo ya Jumanne.

Matokeo hayo yalitangazwa huku majimbo saba yakiwa bado kura zao kuhesabiwa, lakini maofisa wa uchaguzi wamesema Banda hatoweza kumfikia Sata.Habari katika mitaa mbalimbali nchini humo, zinasema kuwa wasiwasi uliogubika matokeo hayo ulisababisha makelele huku wafuasi wa Patriotic Front wakishangilia ushindi wao.

Maelfu ya watu walifurika nje ya geti lenye ulinzi mkali wakipiga ngoma, wakipiga honi na kupeperusha bendera.

Tuesday, September 27, 2011

LEO KWENYE MAAJABU YA DUNIA


Huyu ni Mbwa mdogo tena wa ndani ya nyumba aitwae PUGGY mwenye umri wa miaka 8 aishie Stanford Hill hapa Central Londo. Mbwa huyu ni mdogo kwa umbo ila ndie Mbwa mwenye 'ULIMI' mrefu kuliko Mbwa wooote Duniani wanaoishi sasa! Ulimi wake una urefu wa inchi 4.5

SOMA HAPA CHINI, JINSI YA KUEPUKA KUWA MWAUME 'SURUALI'...




MWANAMUME ni kichwa cha familia, kwa maana ndiye kiongozi katika familia. Hakuna ubishi kuwa kiongozi akiwa wa hovyo, wengine watakuwa na wakati mgumu kuwa na maendeleo. Inasikitisha kwamba kuna watu wako kwenye ndoa wanatesana badala ya kupeana raha. Kuna wanaume wanawatesa wake zao, kisa wana vimada nje ya ndoa. Kuna wanawake nao wanao wanaume wengine, ndani ya ndoa ni jeuri tupu, ukweli ni kwamba haya yote ni ujinga. Katika maisha mume na mke wanapaswa kufahamu kuwa wanalo deni la kupendana. Katika ndoa ni lazima uwe makini na kauli na matendo yako. Usipendelee kuongea kauli ambazo ukiambiwa hautazifurahia. Maisha sahihi katika ndoa ni pamoja na kila mmoja kujiona kuwa analo deni la kumtendea mwingine lililo jema. Je mkeo unamtendea jema gani? Kuna wanaume wengi, kwa nje wanaonekana wazuri, lakini wanawatesa sana wanawake zao. Nimekuwa nikitoa ushauri wa ana kwa ana na kuendesha semina kila jumamosi za masuala ya ndoa, kati ya kero kubwa katika ndoa ni wanaume kuwa na roho mbaya, wanawanyanyasa wanawake kwa matendo na hata wakati mwingine kuwapiga. Kasi ya wanaume kuwapiga wanawake imepungua huenda ni kwa hofu ya sheria, bado kuna wanaume wamekuwa wanyanyasaji, kwa mfano wa kauli chafu, anarudi nyumbani amelewa halafu analazimisha tendo la ndoa wakati ananuka jasho. Hii si sahihi hata kidogo. Mwanamume kurudi nyumbani umeshashiba si hekima, kurudi nyumbani usiku wa manane kwa sababu umetoka kwenye uchafu wako. Wengine wanapokuwa wametoka nyumba ndogo, wanaingia kwa wake zao kwa fujo na makelele, mbona nyumba chafu!!! Eeeh utatoka hapa!! Yamekujaje haya, kumbe anafanya hivyo mke asiweze kuhoji mbona unanuka harufu ya kondom, au mafuta ya kike nk. Unajiona mjanja, kumbe ni ujinga. Kuna wanaume wako tayari kuwaendeleza nyumba ndogo,si wake zao. Huu ni upumbavu. Ndugu yangu vipi una akili kweli? Huna. Angalia vizuri matendo yako. Ni aibu mzazi kuruhusu watoto wake kutosoma au kutofanya mambo mengine ya maendeleo. Mwanamume kweli (si mwanamume suruali), hufanya mikakati ya kuhakikisha watoto na familia yake inakuwa na maisha yanayofaa, wanakula, wanavaa, wanasoma na wakati fulani kupata nafasi ya kuzungumza na watoto au mkewe. Je wewe mara ya mwisho kujadiliana na mkeo ni lini? Chunga sana maisha yako, fainali uzeeni. Unawekeza fedha kwenye gesti, unawekeza fedha kwenye ulevi na anasa, jua unajiharibia mwelekeo wa maisha yako mwenyewe. Jua kwamba utavuna unachopanda. Haiwezekani, upande bangi utarajie kuvuna mpunga!!! Mwanamume pia unapaswa kuwa makini katika suala zima la afya; ni makosa kwa mfano kula tu ili mradi, bali unatakiwa kujua hiki nakula kwa ajili ya nini. Hivi sasa kuna kasi kubwa ya wanaume wenye tatizo la nguvu za kijinsia, mojawapo ya sababu ni ulaji usiofaa. Zipo sababu zingine kama vile kujichua, mikwaruzo katika mahusiano, kuwa na mpenzi asiyejua mambo, uvutaji sigara na ulevi au kufanya mazoezi kwa muda mrefu kisha kuacha, kwa asilimia kubwa vyakula vinachangia. Ziko dawa za kutibu kabisa tatizo la nguvu za kijinsia kama nilivyozungumzia hivi karibuni, huna sababu ya kulia, badala yake unapaswa kuchukua hatua, kwani ushindi haupatikani kwa kulia, bali kwa kuchukua hatua kupambana na kile ambacho kinakusumbua. Amka ndugu yangu, cha msingi katika maisha ni kupambana na kile kinachokusumbua, kwa hakika mwisho utashinda, na ndoa yako itakuwa nzuri. Kuepuka kuitwa �mwanamume suruali� unapaswa kuwa mwanamume kweli unayejua majukumu yako na kuyatenda kwa vitendo, unapaswa kuwa imara kwa kila kitu kuanzia uchumi hadi mahaba, tafiti zinaonyesha kuwa wanawake wanahitaji wanaume rijali, si goigoi!!! Si kwamba kwao hakuna chakula, ndio maana amekubali kuwa nawe, wanahitaji mengine na hilo pia, kama ambavyo wanaume wanahitaji!!!

HUYU NDIE MCHEZAJI WA KWANZA AFRIKA MASHARIKI KUCHEZA SOKA ULAYA...


Huyo bwana anaitwa SUNDAY RAMADHANI MANARA aka 'Computer' aliyezaliwa miaka 54 iliyopita mjini Kigoma mahali ambapo palikuja kuwa chimbuko la wachezaji wengi nyota kama akina Hamis Askari, Aloo Mwitu, Athuman Juma, Juma Kampala, Abeid Mziba, Makumbi Juma na wengineo.
Mkongwe huyo, ambaye ndugu zake wawili nao walikuwa wanapiga soka yaani Kitwana Manara kaka yake na mdogo wake Kasimu Manara kwa sasa anapatikana maeneo ya Temeke, jijini Dar es Salaam.


MAISHA YA UTOTONI KATIKA SOKA
Sunday anakumbuka maisha yake ya utotoni alianza kuchezea Young Kinya ambayo ilikuwa kama timu ya watoto wa Yanga ingawa ilikuwa kama inajitegemea zaidi na ilikuwa inafanya mazoezi nje ya viwanja vya Kaunda na ilikuwa ukitoka pale unasogea kidogo unakwenda Afrikan Boys ambayo ilikuwa ni timu ya pili ya Yanga na mwanzoni mwa miaka ya 1970 Sunday na wenzie akina Awadhi Kessy, Douglas, Shabaan Ufunguo, Mohamedy Ugando walipandishwa kuichezea Yanga ya wakubwa chini ya kocha Profesa Victor Stanculescu na huko waliwakuta kina Elias Michael, Mohammed Msomali, Hassan Goboss, Boi Iddy, Athuman Kilambo, Maulidi Dilunga, Badi Salehe, Leonard Chitete na wengineo.

MALEZI YAKE KWA STANCULESCU
Sunday, ambaye binafsi anakiri kuwa hajui jina la mashine hiyo yenye kufanya kazi vizuri alipewa na nani zaidi ya kukumbuka tu ni mwaka 1975 alipotoka Zanzibar baada ya kuwapiga Simba mabao 2-0 ila anakubali kuwa maisha waliyokuwa wanalelewa na Mzungu huyo yalimfanya aipende sana Yanga kuliko timu nyingine yeyote ikiwamo Taifa Stars, ambayo walikuwa wachezaji takribani saba, ambao ni kipa Elia Michael, Athuman Kilambo, Hassan Gobboss, Abdulhaman Juma, Kitwana Manara, Gibson Sembuli na yeye mwenyewe.
Ushirikiano ulikuwa mkubwa na ulisababisha kuwa mara zote ni furaha tupu ndani ya mitaa ile ya Jangwani hadi mwaka 1973 ambapo Simba ilifuta uteja kwa kuwafunga bao 1-0 lililowekwa kimiani na nahodha wa Simba wakati huo, Haidar Abeid �Muchacho�.

SUNDAY MANARA NA SIMBA
Sunday anasema mara zote alizokuwa akikutana na Simba alikuwa anawaua tu bila masihara, mwaka 1971 Simba ilifungwa mabao 2-0 na moja alifunga yeye na jingine alifunga Maulid Dilunga, mwaka 1974 mechi ya kihistoria ambayo ilipigwa mjini Mwanza katika Uwanja wa Nyamagana, Simba ilifungwa mabao 2-1, yaliyofungwa na Adam Sabu kwa upande wa Simba kabla ya Gibson Sembuli kufunga dakika ya 87 na Sunday Manara kushindilia msumali wa mwisho dakika 30 za nyongeza.
Mechi nyingine ilikuwa ni fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki iliyopigwa mjini Zanzibar katika Uwanja wa Amaan na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, huku goli la kwanza likifungwa na Sunday Manara la umbali wa zaidi ya mita 25 na kusababisha utata mkubwa kwa manazi wa Simba wakimtuhumu kipa wao Athuman Mambosasa kuwa aliachia makusudi au alipewa kitu kidogo na bao la pili lilifungwa na Gibson Sembuli kama kawaida yake kwa shuti kali sana.
Mbali na kuifunga Simba mara zote hizo, Sunday pia alikuwa ni rafiki mkubwa sana wa kipenzi cha Simba, Abdallah King Kibaden Mputa ambaye kwa sasa ni meneja wa Simba.
Sunday pia alioa binti wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Simba, mzee Hassan Haji ambaye ni baba mkubwa wa Mohammed Mkweche aliyekuwa beki maarufu wa Pan African.
Simba pia ndio waliofanikisha mpango mzima wa Sunday Manara kwenda kucheza soka la kulipwa nje ili atoe balaa la wenyewe kufungwa na mtu huyo, huo ndio uhusiano wake na Simba maarufu kama Lunyasi

KUVUNJIKA KWA YANGA KUZALIWA PAN
Sunday akizungumza kwa masikitiko makubwa na bila kumung�unya maneno anamtupia lawama kubwa kocha raia wa Zaire wakati huo, Tambwe Leya kuwa baada ya kutolewa na Enugu Rangers ya Nigeria katika mashindano ya Afrika aliwatuhumu wachezaji nyota akina Sunday, Omary Kapera, Sembuli na wengineo kuwa wameihujumu timu hadi kusababisha kufungwa hivyo wanachama kwa hasira wakawafukuza viongozi wote wakiongozwa na mzee Tabu Mangara na Shiraz Sharif na kuwekwa viongozi wengine ambao waliwataka wakiri makosa.
�Kwa kuwa hatukujua kosa letu, tukaondoka na kuelekea Nyota Afrika ya Morogoro na baadaye tukarudi Dar es Salaam na kuunda timu inaitwa Pan mwaka 1976,� anasema.

SUNDAY MANARA NA SOKA LA KULIPWA

Mwaka 1977 Sunday alitimkia Uholanzi kupiga soka la kulipwa na alikuwa mchezaji wa kwanza Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla kwenda kucheza katika ligi kubwa Ulaya katika timu ya Heracles ambayo ipo hadi sasa katika ligi hiyo na huko alikutana na watu kama akina Jaan Rep, Ruud Krol, Johan Neeskens, Johan Cruyff ,Van Hangem na wengineo. Alikaa huko mpaka mwaka 1979 alipotimkia nchini Marekani ambako walikuwa wameanza mipango ya kukuza soka nchini kwao.

TENGA KAJIFUNGIA NA FIKRA ZAKE
Sunday akizungumzia soka la Tanzania anamshushia lawama nzito Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Leodegar Tenga kuwa analipeleka soka kuzimu na kuwa hahitaji ushauri kwa watu ambao anajua kabisa kuwa wamecheza soka kwa upeo mkubwa na soka wanalielewa kama yeye.

�Tenga hapendi kukosolewa sasa mawazo mapya atayapata wapi? Namshauri kama mdogo wangu aitishe mdahalo wa kitaifa tuzungumzie soka, tupo tunaojua matatizo ya soka si hao wenye vyeti na soka hawalijui,� anasema Computer ambaye kwa sasa yuko mbioni kuwa na Academy yake ambayo itakuwa mfano wa kuigwa nchini

SOKA LA ZAMANI NA SASA
Computer anasema viongozi wa zamani walikuwa na mapenzi makubwa na viongozi wenzao wa timu nyingine na wachezaji wa upande mwingine pia wachezaji walikuwa wanapendana nje ya uwanja, upinzani ilikuwa ndani ya uwanja.

Sunday, ambaye ni mpenzi wa Barcelona ya Hispania anawasifia wachezaji kama Mbwana Bushiri, Emil Kondo na John Lyimo kuwa walikuwa na vipaji vya hali ya juu, ingawa anakiri kuwa hata sasa wapo wenye vipaji lakini wameshindwa kuvumbuliwa.


NAWATAKA 'RADHI' WADAU...

Kumradhi wadau wa KINYAIYA'S BLOGU, nilikuwa kimya kidogo hapa Bloguni kutokana na kusafiri sehemu tofauti na ivyo muda wangu kuwa 'FINYU' kwakweli ila nawaahidi kuanzia kesho Juma5 ntaanza kuwaporomoshea 'MAVITUZZ' kama kawa hapa Bloguni, Stay tune...

Saturday, September 17, 2011

NAWATAKIA WEEKEND NJEMA WAPENZI WA KINYAIYA'S BLOGU...


Jamani nawatakieni Weekend njema na kwa wale wanaoniandikia 'Comments' zao kwamba wanajaribu kunipigia kwa namba yangu ya apa UK alafu hawanipati ni WAONGO! Sasa namba ni hiyo hapo kulia kwenye Profile Picha ya Blogu, jaribu uone...

Friday, September 16, 2011

HUU NDIO MOTO WA TWANGA PEPETA JANA ALHAMIC USIKU PALE MAISHA CLUB OYSTERBAY JIJINI DAR...


Bendi ya TWANGA PEPETA kama kawa jana ilizingua watu ndani ya ukubwa wa MAISHA CLUB jijini Dar kwa burudani nziti kama kawaida yao! Picha Rapa MSAFIRI DIOUF akimwaga Ghani kali stejini, kushoto ni SEMSEKWA...

Mnenguaji MARIA SOLOMA akinengua vikali na mwimbaji Nguli wa Bendi hiyo SALEH KUPAZA...

Mnenguaji mkongwe LILY INTERNET akiwaongoza 'Wadogo' zake kumwaga 'UNO' la kufa 'Ngamia' stejini...

Kiongozi wa Bendi ya TWANGA PEPETA, mwanamke wa Chuma LUIZA NYONI MBUTU akiwaongoza wanenguaji wake kwenye 'SHOWBIZ' ya Hatwariii...

Rapa mpya wa Twanga aitwae J4 ni 'matata' sana na anakuja juu sana sasaivi endapo hatalewa sifa...

WAKATI SIE TUKISAKA MLO MMOJA KWA SIKU, MESSI ANA GARI LA BIL 1.4 MTAANI DUUH...


Wakati weye ndugu yangu KAJA.... nani ukiangaikia pesa ya mlo mmoja kwa siku, BINADAMU mwenzetu LIONEL MESSI yuko Barabarani akitembeza MKOKO wake wa bei mbaya huo hapo juu aina ya FERRARI SPIDER 799 wenye thamani ya sh Bilion 1.4 daah...

Huyu DOGO hobbie yake kubwa ni kuendesha Magari pamoja na kucheza Soka la Ufukweni kila anaporudi kwao ROSARIO nchini Argentina...

Ni mfuasi mkubwa wa DIEGO MARADONA na anakiri kwamba alipokuwa mdogo alipania sana kucheza kama Mkongwe huyo wa Soka kwakua nae alibarikiwa kutumia zaidi 'GUU' la kushoto na kuweka 'Nadhiri' moyoni kwamba ni lini atakuja kumwona na kumsalimia Maradona achilia mbali Kumkumbatia kama wanavyoonekana hapo juu, maana hata uso wake unaonyesha kufurahia sana kuwa karibu na mtu wa 'Ndoto' yake kwenye SOKA...

Jamaa ana makaka wawili waitwao RONDRIGO na MATIAS pamoja na dada yake wa pekee aitwae MARIA! Wakati anaanza soka alikumbwa na ugonjwa unaosababisha matatizo katika ukuaji wa mwili uitwao Growth Hormone Deficienty ila wakala wa zamani wa Timu ya Vijana ya Barcelona CARLES REXACH aliamua kuongea na wazazi wa Messi kwamba watamgharamia matibabu yake Ulaya kwa makubaliano ya kuichezea Timu yao ya Vijana baada ya kugundua kipaji chake cha ajabu! Baba yake alikuwa ni Mfua chuma viwandani na mama yake ni Mfanya usafi maofisini ivyo walikuwa 'TAABANI' kiuchumi wkt huo ila kwasasa ni mmoja kati ya wasoka matajiri zaidi Duniani na ni wa pili kulipwa kiwango kikubwa cha mshahara Duniani nyuma ya SAMUEL ETOO wa Cameroon daaah ama kweli soka bwana, sasa sio mwanao anapenda Soka alafu we mzazi humpi ushirikiano wowote utakuwa UMEFELI...

Kama kawa kama dawa ugonjwa wa kuendesha Magari ndio umemtawala huyu Dogo na hapo akiwa na 'Kaka' yake MARCHERANO haaooooo kitaani...

KWAKUA ANAPENDA KUOGELEA, AKIWA FREE ANAENDAGA KUOGELEA NA MPENZI WAKE ANTONELLA ROCUZZO...

Thursday, September 15, 2011

KWANI NI KOSA KWA HUYU BWANA KUJICHONGEA 'MSALABA' WAKE JAMANI...



Nilipoamua kuitoa habari hii ya Gilbert Paul na Msalaba wake hapa Bloguni sikutegemea kuwa ningeweza kutumiwa ujumbe kutoka kwa wadau mbalimbali na wengi walimpongeza sana msanii huyu kwa kuanzisha mada kuhusu kifo lakini kwa nia ya ubunifu kabisa ya kujichongea msalaba wake. Kama msomaji aliyesema hilo ni jambo jema kwani hata dini yake ya Kiislamu inaunga mkono dhana ya kujiweka tayari na kifo.

Lakini kuna msomaji wangu mmoja aliandika barua pepe ndefu na nimeona bora leo nimpe nafasi kwenye Blogu hii ili naye asomwe na wananchi wenzangu ili kuendeleza mjadala.

“Nimeguswa sana na makala yako ya leo ya kwa habari ya bwana Gilbert Paul. Hongera sana kwa jicho lako kuona hilo na kutufikishia wadau kujua hisia za watu wengine. Tumezoea kuona habari za wasanii, nyingi zikiwa za watu wa DAR ES SALAAM kwani ndiyo imani ya wengi kuwa DAR ES SALAAM ndio kwenye kila kitu kumbe hata mikoani kuna wasanii wabunifu zaidi hata kuliko baadhi ya waliopo DAR ES SALAAM isipokuwa hawapati nafasi ya kuonyesha uwezo wao kwa vyombo vya habari ambavyo karibuni vyote vipo huko DAR ES SALAAM.

“Kwa kuwa bwana Gilbert ni msanii katika fani ya uchoraji aliamua kujitangaza katika style (mtindo) yake ya kipekee ambayo ilimgusa kila mmoja, na pengine huyu bwana hakuwa na mawazo kabisa ya kujitabiria kifo chake isipokuwa jamii inayomzunguka (lakini hiyo ) ilikuwa ndio iliyotafsiri ya hilo.

“Sisi waafrika katika mila zetu nyingi kuna baadhi ya vitu tumewekewa imani vikijadiliwa au kuwekwa katika maandishi basi inaonekana kuwa ni uchuro kwa mtu husika, alichokifanya Gilbert hakina tofauti na mzazi aliyeamua kuandika wosia, kwetu huwa ni suala gumu sana kwa mzazi kufanya hivyo na akifanya hivyo huwa ni siri kubwa na ikigundilika kwa watoto basi mzazi huufuta mara moja. Hii hutokea mara nyingi.

“Pia bila kujali imani yako watu wanatabia ya kupenda kuyafanya na kuyatenda yale tu yanayofurahisha nafsi zao, mfano dini karibu zote zinakataza zinaa, lakini kuna baadhi ya watu wanafanya zinaa kiasi kwamba watu wanamzunguka walijua hilo na halipingiki kuwa zinaa ni chanzo kikuu cha ugonjwa wa ukimwi.

Je nikuulize Bw. Ben umesha wahi kuona jamii inamkimbia au kumtenga mtu wanayemfahamu kuwa anazini sana? Tena akiwa mwenye kipato kila mtu atataka awe karibu yake. AU makahaba waliojaa katika mabaa na majumba ya starehe mbona hawakimbiwi ndio kwanza wanakimbiliwa mpaka wakianza kuugua ndio kila mmoja anaanza kujiweka pembeni.

Maana yangu katika "paragraph" hii ni kuwa bw. Gilbert amewasilisha hisia zake katika jamii kulingana na kazi yake, lakini jamii imemsukuma katika mahali ambapo sipo. kwa wale waliomnyima kazi kwa kuona msalaba wana uhakika gani kwa mfano kuwapelekea kazi wale ambao yawezekana ni wazinifu wa kupindukia ambao maisha yao yapo hatarini zaidi ya Tangazo la bw. Gilbert?

Nakutakia kazi njema na BLOGU yako na uendelee kutuletea taarifa nzuri zenye mafunzo katika jamii kama habari hii ya bw. Gilbrt Paul.


Wednesday, September 14, 2011

BABY SHOWER YA BI, SWADDA JUZI MJINI MILTON KEYNES ILIVYOFANA...


Ilikuwa ni Chereko na Hoihoi juzi mjini Milton Keynes kwenye PATI ya BBY SHOWER ya Bi. SWADDA ambayo ilihudhuriwa na 'WATOTO waMUJINI' wootw wa kuanzia London na vitongoji vyake mpaka mikoa ya jirani kama Reading, Coventry na Leicester, ilikuwa balaaa, na Pichani Miss JESTINA akiwaongoza warembo akipouzz na warembe nadnia ya ukumbi wa shughuli....

Mrs MBARUKU na FATMA nao walikuwepo...

MARIAM, VINA na FATMA wakishow Love...

Mduara kwa kwenda MBELEEE...

VINA na MARIAM LASSEKO waliwaongoza warembo wooote wa Mujini waliohudhuria BABY SHOWER hiyo ya Bi, SWADDA iliyofanyika juzi mjini Milton Keynes, mwendo wa saa 1:30 kutoka apa London...

'NONDOZZ' za Mujini kwenye Pouzzzz....

Bi, SWADDA ambaye ndie aliyekuwa mwenye 'SHUGHULI' iyo juzi akiwa kwenye kiti chake cha Enzi huku wapambe wakiwa pembeni kumsubiri 'Mwenzao' aliyeko njiani...

Hapa ni wkt Bi. SWADDA akiingia ukumbini...

SUE KINYAIYA akiwa na MARIAM LASSEKO, ilikuwa raha saanaaaa....

KAMA UNAHISI MWANAO ANA TATIZO LA 'CHOO' SOMA APA CHINI...


Tatizo la kukosa choo watoto wadogo au kuwa na choo kigumu na jinsi ya kulitatua
Watoto wadogo hasa wale ambao bado wananyonya na ndio kwanza wamenzishwa vyakula vinginevyo zaidi ya maziwa, mara nyingi hupatwa na choo kigumu au kukosa choo kabisa hali tunayoiita kimombo, constipation. Hali hiyo huanza pale mtoto anapoachishwa maziwa ya mama na kuanza kunyweshwa maziwa ya kopo au mengineyo au pia anapoanzishwa kula vyakula vingine zaidi ya maziwa. Mara nyingi watoto wanaonyonya maziwa ya mama huwa hawasumbuliwa na tatizo hilo, bali tatizo hilo huanza kujitokeza pale wanapoanza kulishwa vyakula vingine zaidi ya maziwa ya mama. Pia mama ambaye tayari mwenyewe anasumbuliwa na tatizo la kukosa choo, huenda mwanae pia akasumbuliwa na tatizo hilo.
Mtoto mwenye tatizo la kukosa choo huwa anapata choo wa shida huku akisumbuliwa na tumbo na kupata choo kigumu. Wakati mwingine hulia wakati akipata choo huku akijiminya na kukunja uso. Muone daktari iwapo mtoto ana umri wa chini ya mwezi mmoja na hajapata choo kwa siku 4.
Iwapo mtoto wako mchanga au mdogo ana tatizo la kukosa choo au kupata choo kigumu kwanza wasiliana na daktari au mpeleke hospitalini ili upate ushari wa daktari. Pia unashauriwa kujaribu njia zifuatazo:
1. Jaribu kumpa mtoto wako maji safi na salama kuanzia mililita 60 hadi 120 kwa siku. Punguza au ongeza kiasi hicho kwa kuzingatia jinsi hali ya mwanao inavyokuwa. Ni bora maji ya mtoto yachemshwe na kufunikwa vyema.
2. Iwapo maji hayasaidii, jaribu pia kumpa juisi za matunda. Mpe mtoto wako juisi ya tufaha (apple), pea au prune iliyotengenezwa kwa kutumia maji salama na safi kila siku. Anza kwa mililita 60 hadi 120 kwa siku na punguza au ongeza kiasi hicho kwa kuzingatia jinsi hali ya mwanao inavyokuwa.
3. Jitahidi kumpa mwanao chakula chenye ufumwele au fiber. Iwapo mwanao ameanza kula vyakula vigumu, basi mpe vyakula vyenye ufumwele kuliko vyakula vyenye wanga, kama vile tumia unga wa shayiri au tunda la apple na pea lililopondwa pondwa vyema na kuwa kama uji. Epuka kumpa mtoto cereal ya mchele au uji wa mchele kama anatatizo la kukosa choo au kufunga choo.
4. Jiepushe kumpa mtoto wako vyakula vyenye wanga na sukari na vyakula vinavyotengenezwa kwa unga uliokobolewa.
5. Mpake mwanao mafuta kidogo sehemu inayotoka choo kikubwa ili kurahisisha utokaji wa kinyesi. Usitumia mafuta ya madini (mineral oil) au dawa za kulainisha choo na za kuharishwa katika kutibu tatizo hilo la kukosa choo la mtoto.
6. Kukosa choo watoto wadogo mara chache huwa kunasababishwa na magonjwa kama vile Hirschsprung ugonjwa wa kumee neva katika utumbo, au Cystic Fibrosis. Muone daktari au mpeleke mtoto wako hospitalini kama tatizo hilo la kukosa choo linaendelea hata baada ya kubadilisha aina ya chakula cha mtoto au linaambatana na dalili nyingine kama vile kutapika au mtoto kukosa utulivu na kuhangaika.
7. Kuna baadhi ya watoto wanakosa choo au kuwa na choo kigumu kutokana na kutumia maziwa ya ng’ombe. Iwapo umetumia dawa na umefuata maelekezo ya kuondoa ukosefu wa choo na hukufanikiwa. Katisha kumpa mtoto maziwa ya ng’ombe kwa siku mbili au tatu, baada ya siku hizo iwapo bado hajaacha choo badi endelea kumpa maziwa hayo, na pengine tatizo hilo halisababishwi na maziwa ya ng’ombe.
8. Mwogeshe au mweke mwanao katika beseni la maji ya uvuguvugu na hakikisha maji yanafika hadi kifuani. Mkande mtoto tumbo lake wakati akiwa majini na njia hiyo husaidia kulegeza misuli ya mwili wa mtoto, na kumsaidia kupata chook wa urahisi.
N.B Ukosefu wa choo kwa watu wazima baadhi ya wakati huandamana na magonjwa kama vile Arthritis, Appendicitis, Cataract, saratani, shinikizo la damu, Rheumatism na kadhalika lakini kwa watoto huenda tatizo hilo likawa halisababishwi na maradhi hayo.
Utafiti unaonyesha kuwa hakuna uhusiano wowote kuhusu kukosa choo mtoto na kupewa nyongeza ya chuma au Iron Supplement. Hivyo usimkatishe kumpa mwanao chuma iwapo anakosa choo. Kwani chum ni muhimu sana katika kuzuia upungufu wa damu mwilini kwa mtoto wako mdogo.

Monday, September 12, 2011

LEO KWENYE KONA YA MAHABA...


Kwa mara nyingine tena tunakutana kwenye safu yetu hii ya MAHABA!

Rafiki, wanawake wengi hulia na kujutia kuwepo katika ndoa, hii ni kutokana na kuhisi au kujua kuwepo kwa usaliti kwa waume zao. Ukweli ni kwamba suala la kusalitiwa linaumiza sana, hakuna atakayekuwa tayari kukubali usaliti katika penzi lake.

Huo ndiyo ukweli, lakini pamoja na ukweli huo umewahi kujiuliza kwa nini mpenzi wako anakusaliti? Umewahi kufikiri kwamba hata wewe unaweza kuwa chanzo cha mpenzi wako kukusaliti?

Kama hujawahi kufikiri basi fahamu kwamba kama usipokuwa makini katika maeneo fulani katika ndoa yako, unaweza kuwa chanzo cha mumeo kukusaliti. Vipengele vifuatavyo, vinafafanua hilo kwa undani zaidi:

UNATAMBUA MAJUKUMU YAKO?
Hili linawashinda wengi katika maisha ya ndoa na waume zao kwa kukosa kujitambua kuwa yeye ni nani na wajibu wake katika ndoa yake ni upi. Hapo awali kabla ya kuingia katika ndoa na mumeo ulikuwa ukimnyenyekea na kujitahidi kadiri ya uwezo wako kumwonyesha mapenzi motomoto lakini sasa baada ya kuingia katika ndoa umebadilika.

Ulikuwa msafi mwenye kumjali wakati wote na kumwonyesha kuwa yeye ni muhimu maishani mwako na wewe ni muhimu sana katika maisha yake. Kuwa naye karibu wakati wote na kumshauri hasa akiwa katika matatizo na sononeko la moyo au msongo wa mawazo vilimvutia na kuona thamani yako kwenye maisha yake.

Huenda hapo awali ulikuwa mshauri wake mkubwa wa mambo mbalimbali ya kikazi na wakati mwingine mambo yake binafsi, wakati alipokuwa na majaribu ya kufukuzwa kazi au kupata balaa la madeni kazini kutokana na uharibifu au upotevu wa mali ya anapofanyia kazi kwa kumshauri au hata kumsaidia kifedha.

Sababu hizo na zingine nyingi ulizokuwa ukimfanyia wakati mkiwa wachumba huenda ndizo zilizomsukuma akusogeze karibu ili aishi na wewe kwa kutambua umuhimu wako katika maisha yake lakini sasa umebadilika!

Mwanaume anahitaji mwanamke wa kumshauri na kumpa moyo hasa anapokuwa kwenye majaribu na matatizo mbalimbali ya kimaisha.

Kama awali ulikuwa ukimfanyia hivyo mumeo na sasa umeacha ni wazi kwamba atakapokuwa na msongo wa mawazo au matatizo flani atakwenda baa ambako atakutana na mwanamke wa nje na akithubutu kumweleza yaliyomsibu atapata tulizo kwa sababu wanawake wa nje ni mahodari wa kufariji waume za watu.

Baadhi ya wanawake wakishaingia katika ndoa, hujisahau na kuona kuwa wao ni wao na kama walichotaka wameshakipata hivyo kujisahau na kutowapa wapenzi wao mapenzi motomoto. Kikubwa unachopaswa kutambua wewe mwanamke ni kwamba wanaume wanapenda kuona wake zao wanakuwa kwa ajili yao na kuwafanyia vituko vya mahaba kila wakati.

Kadhalika hupenda kuona wake zao wanakuwa karibu nao wanapokabiliwa na matatizo mbalimbali ya kimaisha. Hakika utakaposhidwa kumjali mumeo huona ni afadhali atafute kitulizo kingine ambapo hata hivyo mara nyingi hukimbilia baa kutafuta kitulizo cha msongo wa mawazo.

Wengine hushinda kutwa nzima nyumbani wakihudumia mifugo au wakifanya shughuli ndogondogo za kila siku kama kufua, kupiga deki na kazi nyingine za mama wa nyumbani baada ya hapo hubaki na nguo alizoshinda nazo kutwa nzima hadi mumewe anaporejea kazini humkuta akiwa na nguo hizo chafu huku akinuka jasho ambapo kwa kiasi kikubwa linamkera mume atakaporudi kutoka kwenye mihangaiko yake.

Hivi unafikiri kwa misingi hiyo mumeo ataacha kutoka nje ya ndoa kweli? Kama unakuwa mchafu wakati wote, humfurahishi, huvutii kama zamani unadhani atafanya nini kama siyo kukusaliti?

Lazima utambue majukumu yako katika ndoa yako. Majukumu yako hayaishii kumfulia, kumpasia na kufanya usafi nyumbani pekee! Majukumu yako ni pamoja na kuhakikisha mumeo anafurahia penzi lako pamoja na kumsaidia katika matatizo mengine ya kikazi na kiakili. Anza kubadilika sasa kabla hujampoteza mumeo.

HUYU NDIE GENEVIEVE NNAJI...


Huyu Bidada anaitwa GENEVIEV NNAJI, ni mcheza Filamu nyota wa kike kuliko woote nchini NIGERIA! Alizaliwa mjini MBAISE uliyo katika jimbo la IMO STATE nchini Nigeria mnamo Tar 3 may 1979 akiwa ni mtoto wa 4 kati ya wanane katika Familia yao. Ameshashiriki kucheza Movie nyingi saanaaa na ndie mcheza Filamu anayelipwa pesa nyingi kucheza kwa Filamu moja! Na kwasababu ya Urembo wake ameshafanya matangazo ya Bidhaa kibao kama vile Vinywaji, Sabuni na Mafuta ya urembo!

GENEVIEVE hajaolewa ingawa amebahatika kuzaa mtoto mmoja aitwae JILIET ambaye alimzaa akiwa shuleni na yeye na huyo Binti yake wanafana sana kama huwajui vizuri, hebu waangalie mwenyewe pichani hapo juu wanavyofanana...

Sasa kuna habari kwamba yeye GENEVIEV na mwanamuziki D'BANJ wana uhusiano wa bwana na bibi ingawa wenyewe wanakanusha vikali wkt karibu kila sehemu wanaenda pamoja sasa kwanini watu wasisemeeee...

SASA MCHEC GENEVIEVE KWENYE 'TRELA' YA FILA,MU YA 'IJE'...

Sunday, September 11, 2011

KUTANA NA MWANAMKE WA SHOKA...


BIASHARA ya usafiri wa pikipiki maarufu kama ‘bodaboda’ imeshamiri nchini kote. Hata hivyo, kwa kiasi kikubwa biashara hii hufanywa na wanaume. Lakini hali ni kwa Maria Chacha (25). Huyu ni mwanamke pekee anayetoa huduma ya usafiri wa bodaboda katika eneo hilo. Pamoja na changamoto kubwa anazopata katika kazi hiyo, Maria ameweza kusimama imara na kujipatia riziki yake ya kila siku kupitia kazi hiyo na kuweza kutunza familia yake ya watoto wanne. Maria anasema haikuwa rahisi kwake kupata kazi nzuri baada ya kuachana na mume wake, hivyo akalazimika kutafuta kazi itakayoendana na elimu yake. Kutafuta kazi Anasema awali, alipata kazi hiyo ndani lakini aliacha baada ya siku mbili tu tangu kuanza kutokana na kile anachosema ni ukorofi wa mwajiri wake. Baada ya hapo alianza kazi ya kubeba zege katika jengo lililokuwa likijengwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando anadai kwamba, alikuwa akilipwa ujira wa Sh3, 000 kwa siku. Hata hivyo ugumu wa kazi hiyo ulimfanya aanze kufikiria kazi nyingine na alipata kazi ya ulinzi katika Kampuni ya Ulinzi ya Mara Security na kudumu kwa miezi mitano. “Kazi ya ulinzi ilikuwa ngumu sana kwangu, sikuweza kukesha usiku, tena nje, niliugua sana malaria kutokana na mbu na baridi kali la usiku,” anasema Maria. “Pia gharama za maisha zilikuwa kubwa kwani wakati huo nilikuwa nikiishi na wanangu wawili, hivyo ilinilazimu kuanza kufanya kazi ya umachinga ambapo mchana nilikuwa nikiuza nguo mitaani na usiku nikienda kwenye lindo,” anasema Maria na kuongeza kuwa baadaye aliamua kuachana na kazi hiyo ya ulinzi. Anasema pia kukatwa mishahara bila utaratibu na kuchelewa kulipwa ni sababu nyingine zilizomfanya aacha kazi hiyo ya ulinzi. Udereva wa Bodaboda Baada ya kuzunguka kwa muda mrefu aliamua kuingia kwenye kazi ya udereva wa Bodaboda. Anasema haikuwa rahisi kama alivyokuwa akifikiria kupata kazi hiyo na alikumbana na vikwazo vingi kimoja wapo ni kubaguliwa kutokana na jinsia yake. “Nilikuwa natembelea vijiwe vya waendesha pikipiki nikawaeleza kuwa nataka kuwa dereva wa bodaboda. Wengi walikuwa hawaniamini kama naweza, hakuna aliyekuwa tayari kunipa pikipiki yake nijaribu kazi hiyo” anasema Maria. Lakini kwa bahati nzuri siku moja alitoke jamaa aliyemtaja kwa jina la Marwa Mgaya na kumpatia pikipiki yake ili aone kama ana uwezo wa kuendesha na kuongeza: “Ilikuwa ni bahati kwangu, sikufanya kosa, kila mtu alistaajabu na huo ndio ukawa mwanzo wa kuaminika.” Hata hivyo anasema awali alikuwa na wasiwasi kwani bado hakuwa na uzoefu wa kutosha wa kuendesha pikipiki, lakini baada ya wiki mbili aliweza kuwa mzoefu wa kutosha kujua mitaa ya jiji na kuanza kuona mafanikio yake baada ya mwaka mmoja. Anakiri kuwa kwa kipindi chote alichokuwa akiendesha bodaboda, hakuwa na leseni, hivyo aliona umuhimu wa kuongeza ujuzi wa kazi yake ambapo alisema alienda kusomea udereva kwa muda wa mwezi mmoja. “Niliingia darasani kwa muda wa mwezi mmoja na nusu ambapo niliugawa muda wangu wa kazi na shule, mafunzo haya niliyapata katika chuo cha udereva cha Lake, na sasa nina leseni ya udereva wa pikipiki na gari” anasema. Changamoto kazini Kuna matatizo mengi ambayo Maria anakumbana nayo akiwa kazini, kubwa ni kutoaminika na baadhi ya wateja kuwa anaweza kuendesha pikipiki, hivyo wakati mwingine wanamkwepa na kwenda kwa madereva wakiume. Mazingira magumu hasa wakati wa mvua, pia jua kali la mchana na kudhulumiwa na wateja wakorofi wakati wa malipo ni changamoto nyingine anazokabiliana nazo. Matarajio ya baadaye Maria anasema hajaridhika kuishia kuwa dereva wa pikipiki bali anataka kuwa dereva wa magari makubwa akiamini kuwa kazi hiyo itamuongezea kipato. Aidha Maria aliomba mtu yeyote anayeweza kumpatia kazi ya udereva kwa kipindi hiki tofauti na pikipiki ampatie kwa kuahidi kufanya kazi kwa uaminifu. Historia yake Maria Chacha alizaliwa katika kijiji cha Nyangoto, wilayani Tarime mwaka 1986 akiwa mtoto wa nane katika familia ya watoto tisa wa mzee Samburu Chacha na mkewe Bokhe. Alihitimu darasa la saba mwaka 2001, na mwaka uliofuata aliolewa na Grabriel Chacha aliyeishi naye kwa miaka nane na kuzaa watoto wanne. Mwaka 2009 ndoa yao ilivunjika kutokana na matatizo ya kifamilia baada ya mumewe kumfanyia vitendo vya unyanyasaji, ikiwamo kumpiga na kisha kumfukuza. Baada ya hapo aliamua kuhamia jijini Mwanza na kuanza harakati za maisha.

Saturday, September 10, 2011

HAYA NDI MAMBO KADHAA USIYOYAFAHAMU KUHUSU 'KOFFIE OLOMIDE', YASOME CHINI APO...


Anaitwa kwa jina Halisi la CHRISTOPH AGBEPA MUMBA ANTOINE aka tumezoea kumwita KOFFIE OLOMIDE, mzaliwa wa Kisangani kule Congo ya DRC mnamo Tar Aug 17 1956. Na hapa leo nakuletea mambo kadhaa usiyoyajua kuhusu Koffie.

Koffie amezaliwa kwa Baba mkongo na Mama yake ni raia wa Sierra Leone! Jamaa Hobbie yake ni kuendesha Magari tangu utotoni na aliwaza kuwa mwendesha magari ya Mashindano ila akakutana na ukali wa Babake aliyemwambia 'KITABU' kwanza magari baadae! Koffie ana majina mengi sanaa ya Utani ila kwa leo ntakutajia machache tu kama vile LE GRAND MOPAO, LE SHAKE SPEAR DU ZAIRE, NKOLO LUPEMBA, GRANIBANE MAJI, KADRA KORAMAN na mengineyo mengi tu!

Baba yake mzazi ni mgonjwa kwasasa na anaishi aris Ufaransa wkt Mamam yake ni Dalali wa Madini kule Kisangani mjini. Koffie ana kaka yake mkubwa kuzaliwa aitwae JONNY KO na huwa anamtajaga sana kwenye Nyimbo zake! Jamaa ameoa na ana watoto saba mpaka sasa waitwao, ARISTOTE, ELVIS, MINOU MISS UNIVERSE, DIDIE STONE NIKE, ROCK, DEL PIERO MOURIHNO na SAIT JAMES ROLLS!

Ukitaka kumwalika Koffie kimuziki basi ujue Hotel atakayolala yeye basi na wacheza Shoo wake wa kike nao watalala hiyi hiyo ya bei mbaya, na hilo nimeshalishuhudia kwa macho yangu alipokuja Bongo kwa mara mwisho kutumbuiza maana anawachunga sanaa mabinti hao ingawa inasemekana alishatembea na baadhi yao ingawa 'SKENDO' kubwa iliyoko sasa ni tuhuma kwamba 'anatembea' huyo mwimbaji wake hapo juu kwenye picha aitwae CINDY na kuibua ugomvi mkubwa kwa mkewe alie juu pichani kutishia kuomba 'TALAKA' baada ya kusikia Binti huyo ana Mimba ya Koffie!

NAUPENDA WIMBO HUU WA 'CHOCOLATE YA PAPAA' WA KOFFIE OLOMIDE, NI BALAA...

HILI NI ONYO KWA MAKONDA WOOTE...


Ule mpango wenu kwa kukatisha 'RUTI' alafu mnakuwa wajeuri hamtaki kurudisha Nauli za watu au kuwaambia abiria wahamie Bus lingine siku mkikutana na 'WABISHI' kama hawa jasho litawatoka sheenziiiii...

JAMANI 'WAMACHINGA' MPAKA ULAYA WAPO ILA KWA UTARATIBU MAALUM...


Jamani msidhani 'WAMACHINGA' wapo africa tu ila hata uku Ulaya pia wapo tena wa kumwaga sema wapo kwenye maeneo yaliyopangwa tu, sasa tatizo liko kwa wamachinga wa kwetu Africa wakipangiwa sehemu zao ili uharibifu wa mazingira upungue ni vita daaah! Yaani sisi mpaka tukae sehemu kwa utaratibu itachukua muda sana nakwambieni, na hapo kwenye picha msione NIMENUNA ni kwa sababu kuna Mturuki wa Bucha kaniulizia kuku wa 'Kiswahili' kwakua kaniona mie Mwafrica wkt mie nilitaka kuku wa Kizungu ambaye analainika 'Viungo' Fasta aaaagh...

Kuna pia wauza simu kama mnavyoona na tena wanajua kupiga 'DEBE' hao 'Ova' kariakoo duuuh...

Aaah mbona mambo mulemule 2 jamani...

Hii sehemu inaitwa BRIXTON, ipo katikati ya hapa London ila mtaa tu umetengwa kwa wamachinga pekee na wauza Nyama...

Thursday, September 8, 2011

KUTANA NA BINADAMU MWENYE 'DOMO' KUBWA KULIKO WOOTE DUNIANI KWASASA...


Yaani unaambiwa baada ya kushinda kwa Style yake ya kumeza Kopo la Soda basi Kampuni ya soda ya COCACOLA hapohapo ikampa Dili la TANGAZO na akachukua MKWANJA mreeefuuuuu wkt alikuwa hana raha kule kwao Angola kwa kutaniwa na DOMO lake kubwa na kuambiwa akialikwa kwenye Part atamaliza MSOSI woote na hata mademu walikuwa wanamdic, lakini kumbe mungu kumpa kilema icho ndio kimemtoa kwenye Maisha baada ya kupata pesa nyingi kuitangaza Cocacola na hilohilo DOMO lake haaa haaaa, ama kweli usijione una kilema flani ukachukia jua mungu ana sababu yake bana...

HEE JAMANI HATA 'NAULI' HUNA, JE USINGENIKUTA...



Haa ahaaa maana sina budi kucheka ninapowahadithia kisa hiki wkt nikiwa Bongo wkt natoka kuwatembelea ndugu zangu flani ivi kule Mbezi ila sasa
Wakati nataka kuanza safari ya kurudi zangu home nilikutana na watu wawili; msichana na mvulana wanajibizana. �Yaani hata nauli haunipi, aaah simu yangu haina hata vocha, sasa wakati unaniita ulitegemea mimi fedha ya kujia huku naipata wapi?� ni kauli hii ilitoka kwa mwanamke. Niliwasikia kwa umakini mkubwa, baadaye kwa sababu najuana na mmoja kati yao, niliwafuata, nikajitambulisha, wote wakasema aaah kumbe ndio wewe, nimekuwa nikisoma makala zako kwa zaidi ya miaka kumi sasa, nashukuru sana una ushauri mzuri. Kwa namna walivyokuwa wakizungumza ni kwamba hawakuwa wanajua kama nilikuwa nimesikia namna walivyokuwa wakigombana. Mwanamke anagombania apewe nauli ya kurudi kwao. Ikabidi niwaambie ukweli kuwa niliwasikia walichokuwa wakikizungumza na kwamba sikufurahishwa nacho. Ndipo mwanaume akaanza kusema �Aaah bora umesema, huyu binti bwana ninataka kumuoa, nikamwambia leo kwamba napenda tukutane kwa ajili ya mazungumzo, nashangaa wakati tunaagana analazimisha nimpe nauli wakati mimi mwenyewe kazini hatujalipwa mshahara�. Mikasa ya aina hii ni mingi, kuna wasichana wanaanzisha uhusiano wakiwachukulia wanaume kama mashine za kutolea fedha (ATM). Msichana katoka kwao vizuri, kurudi ni lazima apewe nauli, tena kwa kuomba, hekima iko wapi? Kama una mpango wa kuoana na msichana na anachokiangalia zaidi kwake ni fedha, ni muhimu kupata muda zaidi wa kumchunguza.Kuna wasichana wengine ukiwa naye kwenye daladala yeye ana sh10,000, mwanaume ana sh2000, bado atataka mwanaume ndio alipe nauli.Sijui kosa ni kwanini amemtongoza, huwa sielewi. Kuna wasichana akiwa na mwanaume anamtegeuza mtaji, shida zake zote zitakwisha kwa huyo mwanaume, tena wakati mwingine kwa kulazimisha. Mizinga kwa kila kitu. Eeeh kama uko naye kuanzia chakula, maji, soda na kadhalika, yeye ni mtu wa kula tu, tena wengine wanaweza kukujia hadi na marafiki zake, akukomoe vizuri kwanini umekubali kumpenda. Anakuingiza gharama, wengine unakuta eti hawanywi vinywaji vya bei rahisi. Haya ni maisha ya kipuuzi ambayo ni lazima watu waondokane nayo, maana ya mapenzi ni kusaidiana na kufanyiana mambo ambayo wewe ukifanyiwa utajihisi raha, sio kufanyiana mambo ya kukomoana. Kununuliwa kila kitu ni aibu, kuna wengine wanafanya kazi, lakini fedha zao ni zao na zile za wanaume wao nazo wanataka ziwe zao. Huu ni wizi wa waziwazi. Kama ni suala la kukosa nauli, unapaswa kusema kabla ya kuja. Wasichana wengine ukiwa nao ni matatizo, eeeh kodi ya chumba nilichopanga imekwisha�!!kwa hiyo mwanaume ni ATM? Wakati mwingine huwa sielewi kwanini mwanaume atoe fedha kwa mwanamke, wakati tafiti zinaonyesha hata katika tendo la ngono/ndoa, wanawake ndio wanaopata raha zaidi kuliko wanaume. Unatoa fedha kulipia nini? Ninaowazungumzia hapa ni wale ambao hawako kwenye ndoa, unakuta binti hana kazi ya maana, ana simu ya bei mbaya hata mama yake mzazi hana, hata baba yake mzazi hana, kumbe kamuibia mtu. Je wewe ni kati ya wale ambao kuombwa vocha ni kawaida lakini wanaopigiwa hawajulikani? Ikiwa jibu ndiyo, jua kuwa unaumia. Kivipi? Inawezekana kuna mwingine anayependwa ndiye anapigiwa na wewe unatumikishwa au unaonekana ni pumbavu wa kuibiwa fedha na mali zako. Wapo ambao wanakuwa na sababu za msingi, labda ni kweli anawasiliana na mama yake, labda ni kweli anawasiliana na watu wengine muhimu katika familia yake. Lakini mara nyingi usikubali kuonekana kama ATM. Unaweza kuwa bingwa wa kuhonga, ukifikiri utapendwa, lakini hizo vocha wakatumiwa wengine wanaopendwa. Uwe makini ndugu yangu, achana na vitu visivyo na maana kama hivyo (ngono). Kuna watu wengi wako kibiashara zaidi, ukiwa kwako anasema nakupenda, kumbe kuna watu kama kumi hivi toka asubuhi walishaambiwa nakupenda, usibwete kwa kuamini unapendwa eti kwa sababu umeambiwa. Ni lazima uwe makini na fedha zako. Achana na tabia ya kuhonga, achana na tabia ya ngono, inaongeza umaskini, kwani wasichana wengi kama walivyo wavulana, si waaminifu. Wapo ambao ni waaminifu, ni wachache mno. Ni ujinga pia kumsomesha msichana kwa makubaliano kwamba mtakuja kuoana. Amini ninachokwambia ni nadra sana kuoana naye, zaidi tarajia maumivu. Ni makosa mnapokutana kutoleana ahadi nyingi nzuri. Ni makosa pia unapomkuta mtu kuzungumza juu ya unavyotaka wewe�kwa mfano kuna watu utawakuta wanasema �sitaki Wengi wako kimaslahi zaidi, wako kibiashara zaidi. Ukiwa naye, wako, akitoka tu, ni cha wote�wizi mtupu�fikra ni namna gani naweza kupewa vocha, namna gani naweza kununuliwa chakula cha mchana na mambo mengine yasiyo na maana kama haya. MBINU ZA KUJUA KAMA ANACHOTAKA NI FEDHA AU WEWE; Hebu fanya hivi, kama una msichana ambaye umekuwa ukimtumia vocha, umekuwa ukimsaidia hiki na kile, kuanzia leo hadi mwisho wa wiki hii usimsaidie chochote, halafu uone namna gani atakuwa.
Je unapokuwa hujampa fedha, ukisalimiana naye anaonekanaje? Anakuwa ni mtu wa kuchangamka au anakuwaje hasa? Kwa asilimia kubwa, hata kama labda alikuwa ana kawaida ya kukusalimia kwa kukutumia ujumbe, inakuwa ni mwisho wa salamu hata kama awe na vocha, haki ya Mungu we mjaribu 'DEMU' wa namna hiyo utaona...

Website counter