Saturday, July 24, 2010

'WAGOSI WA KAYA' WATENGANA RASMI...

Binafsi nilikuwa nikiwapenda makaka hawa niliowaona wana AKILI sana kwenye tungo zao kama alivyo Mtaalamu wa Morogoro AFANDE SELE! Lakini nasikitika kusikia makaka hawa waliounda kundi liitwalo 'WAGOSI WA KAYA' kutoka kula mkoani Tanga eti WAMETENGANA! na kisa cha kutengana ni baada ya mmoja wao FREDDY MALIKI aka Mkoloni 'kulia', kuamua kuacha muziki na kujiingiza kwenye siasa na kujiunga na chama cha siasa 'CHADEMA', ivyo mwenzake JOHN SIMBA aka 'Dk John' kuamua walivunje rasmi! Nawakumbuka sana kwa wimbo wao ule wa TFF zamani 'FAT', walinena sana ukweli kwenye ule wimbo daaah...

No comments:

Website counter