Tuesday, April 12, 2011

SIKU WACHEZA FILAMU TULIPOANDAA 'HARAMBEE' YA KUIZINDUA CLUB YETU PALE NYUMBANI LOUNGE...


Watotozzzz wa BONGO MOVIE CLUB wakipata vinywaji kwenye 'HARAMBEE' hiyo ya nguvu iliyofanyika NYUMBANI LOUNGE kwa mshkaji wangu GADNA pale nyuma Best bite Namanga, Ilikuwa ni Harambee maalum ambapo tuliwaita watu 'WAZITO' na wadau na wapenzi wa FILAMU nchini kwa dhumuni la kutuchangia kutunisha mfuko wa 'CLUB' yetu ya wacheza Filamu ambayo inajumuisha Timu mbili yaani Football kwa Wanaume na Netball kwa Wanawake, na wengi waliitikia wito na tunashukuru ingawa michango yenu binafsi na Taasisi mbalimbali tunaomba mtusaidie kutunisha 'mfuko' wetu ili malengo yetu yaweze kutimia...

Mauwa yoote yalikuwepo sikuhiyo na hapa wanaonekana kina SHILOLE, FLORA MVUNGI na wengineo wakifurahia mandhari...

Kikao kikiendelea huku 'vinywaji' vikitembea...

Pichani, mimi RICHIE, CHECBUDDY, WEMA, STEVE NYERERE na FLORA MVUNGI tukiteta...

No comments:

Website counter