Monday, April 18, 2011


Mwimbaji nguli PATCHO MWAMBA aka 'Tajiri' akiwa sambamba na mwimbaji mpya wa kike wa Bendi hiyo aitwae Mariam ndani ya Msasani Club jana Jumapili...

Huyu anaitwa B52, ni mpiga gita la 'Solo' mkongwe nchini ambaye kwa wale wanaomkumbuka mwanamama SAIDA KALORI alivyotamba na zile nyimbo zake kwenye Album ya 'chambua kama karanga' basi huyu bwana ndie mtunzi na mpigaji wa gita katika ile Album yooote na kumpaisha sana SAIDA KALORI, kwasasa yupo na FM ACADEMIA...

Huyu anaitwa Queen Suzy, ni mnenguaji 'HATARI' ila ni bingwa wa kuhama Bendi, na tabia hiyo imemsababishia 'uadui' mkubwa kila anakoenda na 'kibaya' zaidi huwa anatokaga FM ACADEMIA anahamia TWANGA PEPETA, alafu anaondoka TWANGA anarudi tena FM ACADEMIA looh! Sasa ameshahama mara na kurudi maranyingi sana na majuzi alitoroka TWANGA akaenda OMAN basi ile kurudi Bongo akaenda kutua FM moja kwa moja daah...

QUEEN SUZY akiwajibika Jukwaani jana Jumapili ndani ya Msasani Club...

No comments:

Website counter