Thursday, December 2, 2010

HAWA NDIO WATU WATANO MATAJIRI ZAIDI DUNIANI...

Hapa hatuongelei watu wenye 'pesa ya Kula' ila tunawaongelea wale vibopa wa hii Sayari tunayoishi, sio weye mwenzangu na mie ukiwa na vimilioni 'tuwili tutatu' baaasi tabu tupu apa mjini loooh! Huyu bwana apo juu anaitwa CARLOS SLIM HELLU, mzaliwa wa Mexico City nchini MEXICO na ndie mtu 'TAJIRI' kuliko woooooooooote Dunia hii tunayoishi kudaadekiii! Ana umri wa miaka 70 sasa akiwa ni mzaliwa kutoka kwa Baba mhamiaji kutoka LEBANON aliyeingia nchini MEXICO mwaka 1902. Ana utajiri wa kiasi cha Dolla BILLIONI 53.5 alioupata kwa juhudi Binafsi bila kurithi chochote kutoka kokote na ni Mmiliki wa Mtandao wa simu wa TELECOM uliosambaa Dunia nzima! Ana shahada ya Sayansi na Sanaa kutoka chuo kikuu cha Nacional Autonomed MEXICO! huyu mzee ameshafiwa na Mke wake ila ana watoto 6, upo apooo....
Huyu anaitwa BILL GATES 'mzee wa kuku' ambaye wengi wetu tulikuwa tukidhani kwamba bado ndie mtu tajiri zaidi Duniani kwa muda mrefu kabla ya bwana Carlos apo juu kumpiga 'BAO' la kisigino! Ndio mtu wa pili kwa Utajiri sasaivi apa Duniani akiwa na utajiri wa Dolla Billioni 53 na ni mmiliki wa Kampuni ya mtandao ya MICROSOFT akiwa na umri wa miaka 54 na ni mzaliwa wa MAREKANI. Sasaivi anaishi mkule Medina Washington na wala hakumalizia Chuo Kikuu. Jamaa ana mke na watoto 3!

Huyu mzee anaitwa WARREN BUFFETT,ni mtu watatu kwa utajiri Dunia hii na ni mzaliwa wa Marekani mwenye umri wa miaka 79. Ni mmiliki wa kampuni ya BERKSHIRE HATHAWAY mwenye utajiri wa Dolla Billinoni 47 mwenye makazi yake mjini Omaha Nebraska na ni Mhitimu wa shahada ya Uzamili ya Sayansi kutoka Chuo kikuu cha COLUMBIA. Huyu nae ameshafiwa na mke wake ila ana watoto 3.

Huyu ni muhindi aitwae MUKESH AMBANI mweny umri wa miaka 53 mkazi wa Mumbai kule INDIA. Yeye ni mtu wa nne kwa utajiri Duniani na amerithi na kuiendeleza Kampuni ya Familia yake inayojihusisha na Ujenzi na Mafuta. Jamaa ana utajiri wa Dolla Billioni 29 ingawa hakumaliza Shahada yake ya Uzamili katika chuo kikuu cha Bombay kule India na ameona na kupata watoto 3! Sasa fikiria tajiri kama huyu ana watoto watatu amemaliza, sasa weye 'mbongo' mwenzangu kapuku watoto '9' wa kazi gani jamani wakati una njaa inakukabili...

Huyu bwana ni mtu wa tano kwa utajiri Sayari hii na anaitwa LAKSHMI MITTAL, ana umri wa 59 na ni mzaliwa wa INDIA ila makazi yake kwasasa ni jijini LONDON Uwingereza. amerithi Kampuni ya Gesi na Mafuta kutoka kwa Babake, ana umri wa miaka 59 na ni mhitimu wa shahada ya Sayansi na Sanaa kutoka chuo kikuu cha CALCUTTA. Ana utajiri wa Dolla Billioni 28.7 ila fikiria jamaa ana watoto 2 tu, msichana na mvulana Daaah...

2 comments:

Anonymous said...

asante kwakutujuza wengine ambao tulikuwa hatujuii endelea kijana kutuletea habari motomoto ubarikiwe

Anonymous said...

abromovich wangapi

Website counter