Saturday, December 18, 2010

BREAKING NEWZZ, ABUU SEMHANDO HATUNAE TENA...


Mkongwe wa muziki nchini ambaye pia ni Katibu wa Bendi ya TWANGA PEPETA ABUU SEMHANDO el maarufu kama BABA DIANA, pichani kulia, amefariki dunia sasaivi maeneo ya Mbezi kwenye ajali ya Pikipiki aliyokuwa akiiendesha wakati anatoka kazini kwenye onyesho la Bendi hiyo aliyokuwa ikitumbuiza maeneo ya Mbezi usiku huu! Amefariki sasaivi kwa kugongwa na gari aina ya Marcedec Benz lenye namba za usajili T855BLG ambayo baada ya kumgonga na kumjeruhi vibaya kichwani na kumponda dereva wake alikimbia na kuiacha Benz iyo barabarani na maiti bado ipo baabarani mpaka sasa ikizungukwa na wanamuziki woote wa Twanga Pepeta wakisubiri hatua za kuchukuliwa kupelekwa Hospital ya Lugalo. Ni jana tu nilikuwa napiga nae story kwenye viwanja vya Biafra wakati tukiaga mwili wa Dokta REMMY ONGALLA na mada yetu ya mwisho tuliokuwa tukiiongea ni jinsi ule wimbo wa Remmy uitwao kifo ambako kuna kipande Remmy aliimba kwamba 'kwanini kifo hutoi taarifa, maana tungeacha urithi alafu tukufate popote ulipo na wala hatutakulaumu tena kifo weee'! Kwenye picha hii Semhando anaonekana akiwa na ASHA BARAKA na kiongozi mwa Twanga LUIZA MBUTU, mungu ailaze Roho ya marehemu mahali pema peponi, AMEIN.

1 comment:

Anonymous said...

Mwaka unaisha vibaya huu, kwenye kuwakumbuka marehemu leaders alikufa mtu baada ya shughuli kwisha tena kwa ajali, haya Dk Remmy kazikwa kesho yake BaBa Diana kamfuata kwa ajali ile ile Mungu awaweke mahali pema peponi. Kwa kweli ya kwetu hatuyajui ila tujiweke tayari kwa maombi.

Website counter