Friday, October 14, 2011


Ndani ya 'PIPA' kama kawa kuitafuta Bongo kudaadekiii...

Sasa kwa Bahati nzuri Ndege yetu ilipitia juu ya kilele cha Mlima 'KILIMANJARO' na sie abiria tukauona vizuri pale kwenye 'shimo' juu ya Kilele chake! Ilikuwa raha sanaaa na wengi walifurahia kuona kilele cha Mlima huo mrefu kuliko yooote barani Africa...


Na mwisho kabisa ndani ya Ndege juzi nikakutana na rafiki yangu kwa mara ya Pili, naye si mwingine ila ni Kiungo nyota wa timu ya taifa ya GHANA na klabu ya INTER MILAN ya Italia SULLEY MUNTARI, ambaye ingawa alikuwa amelewa kwa Masanga bado alikuwa mchangamfu kwenye maongezi yetu usiku mzima tuliokuwa tunasafiri kwenye ndege yetu na aliniambia anaelekea Nairobi nchini Kenya ila atafanya juuu chini kutafuta nafasi ya kuja kunitembelea Tanzania maana anaisikia tu ingawa hajawahi kufika...

1 comment:

Anonymous said...

tunakumiss sana Northampton ingawa hujatuaga...see ya soon..

Party animals..

Website counter