Saturday, July 10, 2010

RONALDO AMPA JINA MWANAE MCHANGA...


Baada ya kupata mtoto wa kiume majuzi kutoka kwa Mwanamke Mmarekani ambaye hajulikani kabsaa, winga nyota wa Real Madrid ya Spain CRISTIANO RONALDO ameamua kumpa jina mwanae huyo na kumwita CRISTIANO jr! Mara baada ya mtoto huyo kuzaliwa, Ronaldo alimtuma dada yake aende nchini Marekani kumwangalia mtoto huyo wakati akiwa mapumzikoni nchini Urusi kwa Demu wake aitwae IRINA SHAWK na kisha dada kumjibu kwamba amefanana saanaaa na mtoto wake duuh...

3 comments:

Anonymous said...

jamaa umaarufu unamuendesha kishenzi kupata pesa ukubwani kazi kweli kweli tofauti na kuzaliwa nazo na bado atazimika kama De lima inabaki story

KINYAIYAS ENTERTAINMENT said...

Ndiko anakoelekea sasaivi maana kiwango kimeshuka sasa kwa ajili ya Starehe! Ben.

dickdada said...

Achaaa kubania kaka kiwango bado kiko juu jamani..subiriii uone mavituzi yake hapo Real Madrid chini ya mzee special one!Ndioo utajua kama jamaaa ni noma na kwa habarii nyepesi nasikia uyoo CR jnr atakuwa mpiga kabumbu vile vile kwani kachukua miguu ya baba yake!kazi ipooo hapo kaka

Website counter