|                                 |                                         | 
 |                       | 
 
 
 |                       |                            SIMBA sasa inahitaji ushindi wa mabao 2-0  itakaporudiana na TP Mazembe wiki mbili zijazo ili isonge mbele katika  michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.                             |  |                               | 
 |                               |  |                               | 
                                                                         | Habari zinazosomwa zaidi: |                                      
 
 |  |  
 Hatua hiyo inatokana na kipigo cha mabao 3-1 ilichokipata jana  kutoka kwa TP Mazembe katika mchezo wa kwanza raundi ya kwanza Ligi ya  Mabingwa Afrika uliofanyika Uwanja uitwao Stade de La Kenya wenye uwezo  wa kuchukua watazamaji 35,000, ambao ulijaa, huku wenyeji wakiwa na  vikundi karibu tisa vya ushangiliaji.
 
 Ni matokeo ambayo yalipokewa kwa furaha na wachezaji wa Simba  akiwemo Kocha Mkuu, Mzambia Patrick Phiri, ambaye alisema amekubali  matokeo na watajipanga kuhakikisha wanapata ushindi zitakaporudiana Dar  es Salaam na kusahihisha makosa.
 
 Katika mchezo huo, Patou Kabangu aliipatia TP Mazembe bao la  kuongoza dakika ya 11 kutokana na mpira wa adhabu walioanzia na  wachezaji wa Mazembe na kupiga shuti lililomshinda kipa Juma Kaseja.
 
 Dakika ya 24, Narlise Ekanga alifunga bao la pili baada ya  kugongeana pasi na Alain Kaluyitika mbele ya mabeki wa Simba  waliojichanganya na kuukwamisha mpira wavuni.
 
 Simba ingeweza kuwa ya kwanza kupata bao baada ya kuanza mchezo,  lakini ilikosa umakini katika umaliziaji, kwa washambuliaji wake  Emmanuel Okwi, Patrick Ochan, Mbwana Samatta na Mussa Mgosi kushikwa na  vigugumizi vya miguu kila walipokaribia lango la TP Mazembe lililokuwa  linalindwa na kipa Kidiaba Muteba.
 
 TP Mazembe ambao ni mabingwa watetezi wa ligi hiyo, ambapo Desemba  mwaka jana ilikuwa timu ya kwanza Afrika kucheza fainali ya klabu bingwa  ya dunia na kufungwa mabao 3-0 na Inter Milan, ilifunga bao la tatu  dakika ya 66 mfungaji akiwa Narlise Ekanga akiunganisha mpira wa kona.
 
 Dakika 10 baadaye Simba iliyofikia hatua ya kuvaana na Mazembe baada  ya kuiondoa Elan de Mitsoudje ya Comoro katika mchezo wa hatua ya awali  kwa jumla ya mabao 4-2, ilipata bao kwa mkwaju wa penalti iliyofungwa  na Emmanuel Okwi.
 
 Penalti hiyo ilitolewa na mwamuzi Younis Yassek wa Misri baada ya  kipa Kidiaba Muteba kumuangusha Okwi eneo la hatari katika harakati za  kuokoa.
 
 Simba ilizinduka zaidi kipindi cha pili baada ya kufunga bao, huku  kipa wake Kaseja akiokoa michomo kadhaa tofauti na hali ilivyokuwa  kipindi cha kwanza.
 
 Simba: Juma Kaseja, Haruna Shamte, Amir Maftah, Juma Nyoso, Kelvin  Yondani, Jerry Santo, Amri Kiemba, Patrick Ochan, Emmanuel Okwi, Mbwana  Samatta/Nico Nyagawa na Mussa Mgosi/Ali Mohammed.
 
 Mazembe: Robert Kidiaba, Pamhile Mihayo, Janivier Besala, Jean  Kasusula, Joel Kihwaki, Benza Bedi, Patou Kabangu/Given Singuluma,  Narlise Ekanga, Alain Kaluyituka, Rainford Kalaba na Deo Kanda.
 |  |  | 
No comments:
Post a Comment