Friday, December 24, 2010

MBONA MAZOEZINI HAMJI ILA KWENYE KUKATA MISHAHARA NI WA KWANZA LOOH...


Mshambuliaji wa Simba, Mussa Hassan Mgosi


MSHAMBULIAJI wa Simba, Mussa Hassan Mgosi amewataka viongozi wake wasimtafutie sababu kwa kumkata mshahara kwani yeye hafanyi kazi na wao bali kocha Patrick Phiri na Meneja wao Innocent Njovu sio uongozi.

Juzi uongozi wa Simba ulitangaza kumkata asilimia tano ya mshahara wa wachezaji wake wawili Mussa Hassan Mgosi na Adbulharim Humud kwa kosa kufika mazoezini na bila kutoa taarifa kwa kocha wala uongozi wake.

Mgosi alisema kuwa viongozi wanatakiwa wamuweke wazi kama kunasheria mpya wameanzisha na wanataka ianzie kwake kwani wanachosema sio kitu sahihi na hivyo ni njama tu.

Alisema yeye hafanyi kazi na viongozi bali benchi la ufundi likiongozwa na kocha wao na hamekuwa akitoa taarifa kwa kocha kila anapokuwa na dharura ila kwa sasa tangu waanze mazoezi hajawahi kukosa hata siku moja.

''Sijawahi kukosa mazoezi hata siku moja ila kunasiku kama mbili hivi nimechelewa kufika mazoezini, lakini sio kukosa na niliongea na kocha kwa nini nimechelewa'' alisema Mgosi.

Mgosi aliongeza kuwa tangu waanze mazoezi hayo hajawahi kuona hata siku moja kiongozi yoyote ameenda katika mazoezi yao zaidi ya benchi la ufundi hivyo ameshangazwa na kauli hiyo ya kutaka kumchafua iliwatu wamuone kuwa ni mtovu wa nidhamu.

Kwa upande wake hana taarifa yoyote ya yeye kukatwa mshahara kutoka kwa viongozi wake na katika mkataba wake hakuna kipengele kinachoelezea kuwa atakatwa.

Pia Mgosi alizungumzia maandalizi ya ligi kuu mzunguko wa pili kwa upande wake alisema amejiandaa vizuri na anamshikuru Mungu kwa sasa amepona yale maunivu ya mguu yaliokuwa yanamsumbua.

Alisema kwa sasa atanachotaka ni kuisaidia klabu yake kutetea ubingwa na kuwaparaha mashabiki wa timu yake ambao wamekuwa wakisubiri raha hiyo na kutetea kiatu chake za dhahabu.

Hata hivyo alizungumzia kidogo mechi zao za kimataifa alisema kuwa wanajua kuwa wanamechi ngumu mbele yao lakini mawazo yao wamewekea katika mechi ya Morocco ambayo itawawezesha kucheza na TP Mazembe kama wataifunga na kudhidi kuonga mbele.

No comments:

Website counter