Friday, October 1, 2010


Hapa nikifanya Interview na Mwanamuziki anakuja juu kwenye Bongo Flava aitwae LINEX ambaye anatamba sana sasaivi kwa wimbo wake maarufu wa 'MAMA HALIMA WEEE'....

Ni wakati wa 'Live Perfomance' kwa LINEX ili kumaliza Ratiba yake ila kama una Swali lolote kuhusu chipikizi huyu basi nitumia apa Bloguni nami nitamuuliza ili niwezi kukujibu...

Mgeni wangu wa pili ni huyu mshambuliaji wa zamani wA WEKUNDU WA MSIMBAZI SIMBA aitwae EMANUEL GABRIEL ambaye ni mmoja kati ya wafungaji hatari wa Magili kuwahi kutokea nchini! Niliongea nae mengi kwenye kipindi changu cha Jumamosi iliyopita na amesema kwamba wafungaji magoli nchini wameadimika nchini na wachezaji wa sasa hawana mapenzi ya kweli ya Soka! Kama una swali lolote la kumuuliza Gabriel nitumie nami nitamuuliza ili aweze kuyajibu maswali yenu kikamilifu...

Gabriek akiwa amekaa kwenye kiti cha moto tayari kutwangwa maswali na watazamaji walihudhuria Studio live sikuiyo ila kama kawa na kesho Jumamosi usikose kuangalia kipindi changu live TBC1 kuanzia saa 12 kamili jioni...

EMANUEL GABRIEL akitoka nje ya Studio baada ya kumaliza mahojiano...

No comments:

Website counter