Friday, July 2, 2010

WEEWEEE CHEZEA 'MO' NA MZUKA WA NGOMA...


Hapa ndipo ninapompendea Mbunge huyu wa Singida Mjini MOHAMED DEWJI aka 'MO' Yaani jamaa anapenda sana kujichanganya bila kujali chochote!Nani anayekumbuka siku Taifa Starz ilipotoka kumfunga Burkina Faso kwao alipovua shati na kumwaga 'uno' la nguvu kwenye Roli la wazi lililobeba wachezaji wa Starz! Jamaa anapendwa sana na wanachi wa jimbo lake na yeye wala hajivungi kwao, ebu mcheki apa anapocheza style maarufu ya 'kiduku' bila kujali vumbi wala jua linalochoma mida hiyo, hii ilikuwa ilifanyika majuzi mkoani Singida duuh...

2 comments:

Anonymous said...

Benie Kinyaiya mambo vp brother, blog yako ni nzuri naipenda ila maneno katika kuitambulisha picha yanakuwa hayako sawa, mfano hy MO hapa anacheza ngoma ya Kilugha ya Mkoa wa Singida ww unasema anacheza kiduku aaaaaaaaah brother kuwa makini mana blog yako inasomwa na watu wenge, otherwise kazi nzuri

Hadj Drogba "mwana chelsea" said...

BEN!BEN!BEN!UNATUDANGANYA MCHANA KWEUPE NAMNA HII,NI LINI NA WAPI TAIFA STARZ ILIIFUNGA SENEGAL?NATAKA UJIBU MWENYEWE WALA USIIBANE HII COMMENT!KWELI WEWE UKO KIBURUDANI ZAIDI SI SOKA JAPO MPIRA KUUCHEZA UNAUJUA CAUSE NILIWAHI KUKUSHUHUDIA UKILISAKATA GOZI LA NG'OMBE SIKU HIZI LINAITWA JABULANI PALE LEADERZ CLUB BONGO ULIMFUNIKA MPAKA MSHAMBULIAJI MWENYE MISULI A.K.A JEZI NAMBA TISA MGONGONI,ILA KWA HILI LA TAIFA STARZ YA MAXIMO KUIFUNGA SENEGAL NAOMBA NISIKUBALIANE NAWEWE,SI KWELI NOOO BEN

Website counter