Thursday, July 8, 2010

WAMASAI NAO WAZIDI KUFURIKA MJINI DAR...


Jamani kama mnavyojua mjini 'DASLAM' wamasai wanazidi kufurika siku hadi siku baada ya wale waliotangulia mjini kuwaambia waliobaki 'Bush' kwamba apo mjini 'Daslam' pesa iko nje nje kwa izo kazi zao za Ulinzi na Kusuka na kuwasokota mademu RASTA! Unaambiwa hawatumii hata lisaa 1 kabla hawamaliza kukusuka Rasta zako hata ziwe nyembamba kama Chelewa maana wanakuzunguka wamasai 3, na wakikumaliza 2 basi we watayarishie iyo Buku 20 ya fasta then nyanyuka akae mwingine! Kwa taarifa yako kwa siku wanakula vichwa zaidi ya 10, kwaiyo usiviangalie kwa wasiwasiivo vijamaa vina hela sanaa ila tatizo lao wateja wanalalamika kwamba wakati wanasukwa hao jamaa hawavai ki2 ndani kwaiyo 'IKULU' zinakuwa wazi! Sasa kwenye swala la kazi ya ulinzi kidogo sikuizi watu wamepunguza kasi ya kuwaajiri maana naskia sikuizi nao wanajua kula 'Dili; na majambazi, maana we ukishavamiwa, yeye utamkuta uwani kafungwa kamba ya geresha mikononi na miguuni na kapigwa vibao viwili vitatu vya 'Danganya toto' basi ujue UMELIWAA MJOMBAAA...

No comments:

Website counter