Sunday, July 4, 2010

BAADA YA KUMWAGWA EATV, KINGWENDU AIBUKA TENA...

Mchekeshaji maarufu nchini RASHID MWINSHEHE MZANGE aka 'KINGWENDU', baada ya kumwangwa kwenye lile shindano la Comedy star search lililoandaliwa na East Africa TV jijini, ameamua kuwakusanya wenzie na kuanzisha kundi lao liitwalo 'ZE DIGITAL COMEDY' litakalojumuisha magwiji wengine kama vile Mzee Small, Bi Chau, Senga, Pembe na Mzee Majuto! Na amesema kilichofanya aondolewe kwenye mtanange wa Comedy star search ni kwakua waandaaji walitaka wachekeshaji wenye sura mpya! Sasa mie najiuliza mbona kina BAMBO na MTANGA wamechaguliwa jamani? Au kiwango kimeshuka mzee tehee teeheee Mie yangu macho nasubiri kuona itakavyokuwa jamani...

1 comment:

Anonymous said...

yani EATV kutoa Kingwendu wamechemka kishenzi na kumuweka Bambo ndo wameharibi kbsaaaaaa. Hilu kundi la Kingwendu na mzee majuto ndo lenyewe majuto,smal na chau hakuaribiki kitu ila huyu Senga mi simkubali bora Pemba yule nae ni noma yani hapa najua TUTACHEKA eatv to heal

Website counter